Ads 468x60px

Sunday, October 07, 2012

HIVI NDIVYO SERENGETI FIESTA 2012 ILIVYO MALIZIKA JIJINI DAR ES SALAAM JANA, NDANI YA VIWANJA VYA LEADERS CLUB.. SHUHUDIA TUKIO ZIMA HAPA





 


 
 Mwanamuziki kutoka nchini Marekani Rick Ross akiimba jukwaani  usiku huu mbele ya maelfu ya wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake kwenye viwanja vya Lidaz Club,wakati wa tamasha la Serengeti Fiesta likirindima.

 Mkali mwingine wa miduara AT na madansa wake wakilishambulia jukwaa.

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka THT,akiimba jukwaani na shabiki wake.
 Mashabiki wakitaka kuangusha uzio uliowekwa kwa ajili ya usalama.
 Baadhi ya Askari wakijaribu kuweka usalama wa kutosha kwa Mwanamuziki Rick Ross imara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Lidaz Club,kwa ajili ya kutumbuiza kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 201.
 Viwanja vya Lidaz palikuwa hapatoshi hata kidogo.
 Mwanamuziki kutoka nchini Marekani,Rick Ross akijisikia furahaa kuwaona Watanzania wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwa ajili ya kumshuhudia yeye akikamua stejini.
Watu kibao wakiwa ndani ya viwanja vya lidaz club usiku huu.
Msanii wa miondoko ya rusha rohoo a.k.a Miduara,Shilole akijiachia jukwaani vilivyo na madansa wake usiku huu mbele ya umati mkubwa uliofika kwenye viwanja vya Lidaz Club,katika kuhitimisha kilele cha tamasha la Serengeti Fiesta 2012.



Wasanii wa kikundi cha Makomando kutoka THT wakionesha umahiri wao wa kucheza jukwaa.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Dyana pichani akionesha mbwembewe zake kabla ya kukamata kipaza sauti,mbele ya umati mkubwa uliojitokeza kwa wingi usiku huu ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar
Msaniii mahiri wa kizazi kipya,Barnaba Boya kiimba jukwaani huku Dyana na skwadi lake wakionesha mbwembwe zao kama kawa.



Msanii wa muziki wa kizazi kipya Barnaba Boy akiimba jukwaani usiku huu 
Mmoja wa wshindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,Youk Killer akishusha mistari yake nguvi usiku huu,huku shangwe na vigele vigele vikiwa vimetawala.
Mashabiki wakishangweka usiku huu vilivyo.
Mmoja wa washindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,Jo Maker akifloo jukwaani. .

Baadhi ya mashabiki wakijiachia vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012

Mmoja wa wshindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,NeyLee akiimba jukwaani .

Baadhi ya wasanii kutoka nyumba ya vipaji THT wakiamsha amsha usiku huu wakati tamasha la Serengeti Fiesta 2012 likiendelea huku mashabiki na wapenzi wa tamasha hilo wakiendelea kumiminika usiku huu ndani ya viwanja vya Lidaz Club,jijini Dar.
Mmoja wa wasanii chipukizi kutoka kwa THT,akiimba kwa hisia mbele ya umati mkubwa wa watu (haupo pichani),uliojitokeza kushuhudia wasanii wa hapa nyumbani na nje wakitumbuiza katika jukwaa moja usiku huu.
Mmoja wa wasanii chipukizi akinogesha jukwaa la Serengeti Fiesta 2012 usiku huu
The Wacko Jako wa bongo akifanya vitu vyake jukwaani usiku huu
Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake wakiwa tayari ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar usiku huu wakati wa tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea kurindima,huku wakimsubiri kwa hamu mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Marekani,Rick Ross ambaye anatarajia kukamua usikuu huu.


0 comments: