Ads 468x60px

Tuesday, July 09, 2013

GEPF YASAINI KUKOPESHA TZS MILIONI 200 KWA SACCOS-BUGANDO



http://www.gepf.or.tz/images/language_logo.pngMfuko wa akiba ya wafanyakazi serikalini-GEPF- imesaini Mkataba wa kukopesha shilingi milioni 200 kwa chama cha kuweka na kukopa –SACCOS- ya Bugando Medical Center –BMC- kwa lengo la kuwanufaisha wanachama kwa mikopo yenye riba nafuu.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi ya makabidhiano ya hundi ya malipo ya fedha hizo Mkurugenzi Mkuu wa GEPF DAUDI MSANGI amesema mkopo huo ni mwanzo wa upopeshaji wa vyama vya kuweka na kukopa nchini SACCOS hivyo wataendelea kuzikopesha saccos lakini ni baada ya kuridhishwa na sifa za usalama wa fedha zao.

Amesema utoaji huo wa mkopo kwa SACCOS ni hatua nyingine ya kujipanua zaidi ilikuwafikia kila wanachama waweze kunufaika na mfuko wao wa akiba ambao una skimu mbili za uchangiaji kwa lazima na uchangiaji wa hiari na ni kwa muda wa miaka 2 ambapo marejesho yake yatatokana na kukatwa katika mishahara kwa wanachama hadi kukamilika kwa deni hilo.

Naye Mwenyekiti wa chama cha kuweka na kukopa –SACCOS- ya Bugando Medical Center –BMC- CLEMENT KISHOSHA amesema mkopo huo wa shilingi milioni 200 unatarajia kunufaisha wanachama 50 kati ya wanachama 700 ambapo kila mkopaji atakopeshwa kulingana kiasi cha mshahara wake.

0 comments: