Ads 468x60px

Tuesday, July 09, 2013

MAAMBUKIZI YA VVU/UKIMWI YAPUNGUA GAIRO-MOROGORO



http://radiomaanta.com/wp-content/uploads/2013/05/HIV-AIDS-in-Bali.jpgMAAMBUKIZI ya Ugonjwa wa Ukimwi Wilayani Gairo Mkoani Morogoro yamepungua kutoka asilimia 3.2 mwaka 2011 mpaka asilimia 2.7 mwaka 2013.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Severin Lalika kwenye mafunzo ya kuyajengea uwezo mabaraza ya kudhibiti maambukizi ya VVU-Ukimwi wilayani humo yaliyoaandaliwa na tume ya kudhibiti maambukizi hayo (TACAIDS)kutoka wilayani Kilosa .

Warsha hiyo iliyowashirikisha wajumbe wa kamati hiyo toka kata nne,taasisi na asasi mbalimbali zikiwemo za dini na kijamii zinazopambambana na maambukizi hayo wilayani humo inakusudi kuweka mikakati ya kuzikabili changamoto za maambukizi wilayani humo.

Lalika alisema elimu na mafunzo kutoka kwa wataalam mbalimbali ndio sababu kubwa ya mafanikio hayo huku akiwataka wajumbe hao kuzingatia mafunzo hayo ili yawe na tija kwa jamii wakizingatia kuwa ni fedha za wanachi zinazotumika katika mapambano.

Awali Mratibu wa Ukimwi Wilayani Kilosa Delfina Pacho aliwataka wajumbe hao kuzingatia mafunzo kwani yanaumuhimu mkubwa kwa jamii katika kupambana na ugonjwa huo.

0 comments: