Ads 468x60px

Wednesday, July 10, 2013

BOKO HARAM WAHUKUMIWA KIFUNGO JELA NIGERIA

Mahakama moja ya Nigeria imewahukumu kifungo cha maisha jela wanachama wanne wa kundi la Boko Haram kwa kuhusika katika mashambulizi matatu makubwa ambapo walitumia mada za miripuko za viwandani karibu na Abuja mwaka 2011.
http://static.guim.co.uk/sys-images/Guardian/Pix/pictures/2013/5/9/1368128242338/Members-of-the-Boko-Haram-010.jpg
Mbali na hao wanne, mwanachama mwingine wa tano wa Boko Haram amehukumiwa kifungo cha miaka kumi jela na wa sita ameachiwa huru kwa kukosekana ushahidi.

Kundi la Boko Haram linadai kuwa mfumo wa Magharibi wa elimu ni haramu na linafanya mashambulizi yake dhidi ya kila mtu anayepinga fikra hiyo.

Makundi ya kutetea haki za binadamu yanasema kuwa, hadi kufikia sasa zaidi ya watu elfu tatu wameuliwa na na kundi la Boko Haram huko Nigeria, mashambulizi ya karibuni kabisa yakiwa ni yale yaliyofanywa na kundi hilo kwenye shule moja ya jimbo la Yobe la kaskazini mwa Nigeria na kupelekea kuuawa wanafunzi 41 na mwalimu mmoja.

Gavana wa jimbo hilo la la Yobe la kaskazini mwa Nigeria ametoa amri ya kufungwa shule zote za sekondari katika jimbo hilo hadi mwezi Septemba, ili kuepusha mashambulio zaidi ya kundi la Boko Haram kwenye shule za jimbo hilo.

0 comments: