Ads 468x60px

Friday, July 12, 2013

HALMASHAURI YA BABATI YAFUTA LESENI ZA BIASHARA



http://www.mwankama.com/images/Babati.gifHalmashauri ya Wilaya ya Babati vijijini, Mkoani Manyara imefuta rasmi leseni zote za biashara zilizokatwa kwa kipindi cha mwaka 2012/2013 kabla ya muda halisi wa mwisho wa kutumika kwa leseni hizo mwezi julai mwaka huu.

Kwa mujibu wa agizo hilo lililotolewa na Mkurugenzi wa Wilaya ya Babati vijijini Dominic Kweka katika kata ya Bashnet, leseni zote za biashara zilizoishia juni 30 mwaka huuzinatakiwa zikatwe upya kwa ajili ya matumizi ya kuendeshea biashara husika.

Kweka amesema kuwa kila mfanyabiashara anatakiwa kukata upya leseni yake na mwisho wa zoezi hilo ni julai 8 mwaka huu na kuanzia Julai 9 wafanyabiashara watakaokaidi agizo hilo watakamatwa na kufikishwa mahakamani.

Aidha ameeleza kwamba uamuzi huo umetokana na mabadiliko ya bajeti ya Serikali kwani awali ilikuwa ikisomwa kila mwezi juni na mwaka huu imekuwa tofauti ambapo ilisomwa mwezi April, hivyo kubadili mfumo wa ubadilishwaji wa leseni hizo.

Hata hivyo baadhi ya wafanyabiashara katika kata hiyo wamedai kwamba Serikali haikuwatendea haki kwani kabla ya kutoa matangazo hayo ingekaa na nao na kuwaelimisha juu ya jambo hilo.

0 comments: